Piga simu bure kwa kutumia internet kwenye simu na pc yako

Mwandishi Hemedans Nassor

hapa nitajaribu kuwakusanyia application karibia zote zinazotumia network ya 3g (hata wifi yenye speed inafaa). hizi application zitakuwezesha kupiga simu bure na kukatwa hela ya internet tu. so kama una unlimited data ya internet uta enjoy. hizi application hazipigi bure kwenda kwenye simu za mikononi (tigo, vodacom.zantel na airtel) wala mezani (ttcl) bali ni bure pale yule unaempigia naye ana application kama yako. mfano mimi nina skype na wewe una skype tukipigiana ni bure.

Pia usihofu kuhusu hela ya internet itakayokatwa ni ndogo sana. Bundle ya mb50 ya extreme au cheka inaweza kuwezesha kuongea zaidi ya masaa matatu.

NIMBUZZ

031913 1613 pigasimubur1

nimbuzz ni social network maarufu ni inassupport kuchat, magame pamoja na kucall bure. ina faida moja ya kukubali kuingia kwenye device karibia zote. nimbuzz ipo kwenye simu pamoja na computer. Mfano wa aina za simu zinazokubali nimbuzz ni

  • JAVA- hizi ni simu kama nokia na Samsung zinazotumia java mara hzote hizi si smartphone na hufanya mambo machache kama vile nokia asha zote.
  • SYMBIAN- hizi ni nokia smartphone maarufu kama n series na eseries ukiona simu yoyote imeanza na N au E ya nokia jua inakubali nimbuzz
  • ANDROID- hizi ni simu kama Samsung galaxies, htc, lg za touch, sony na Huawei nazo zinakubali nimbuzz
  • IOS- iphone zote zinaingia nazo
  • BLACKBERRY- simu zote za blackberry
  • WINDOWS PHONE- nokia lumia, htc na Samsung ativs zote zinaingia nimbuzz

Ukiangalia juu utaona karibia simu zote zinaingia nimbuzz hii inaifanya iwe maarufu sana katika client hizi za kupigia simu. Ili umpigie mtu simu na nimbuzz inabidi wote wawili muwe mumeidownload. Nimbuzz wana video call kwa pc na baadhi ya handset

Kudownload nimbuzz click hapa https://nimbuzz.com

SKYPE

031913 1613 pigasimubur2

hii ni kama nimbuzz sema haissuport java inakubali simu za symbian iphone(ios) android, blackberry na windows phone pia inakubali kwa pc. hii ina faida nyengine ya kukubali video calling. chakufanya ni wewe kuwa na skype na mwenzako kua nayo then unampigia na kuenjoy free call kuipata click link hapo chini

https://skype.com

VIBER

031913 1613 pigasimubur3

Viber ni moja kati ya application maarufu kwa sasa kwa ajili ya kupiga simu za bure na hawa jamaa wanajitahidi kuifikisha application yao kwenye kila pembe ya dunia hadi visimu vidogo vya asha sasa vininaingia viber. Viber ipo pia kwenye blackberry, iphone, simu zote za android, windows phone zote na Symbian kuipata click link hapo chini

https://viber.com/

TANGO

031913 1613 pigasimubur4

Tango wao hawapo interested na simu ndogo focus yao ipo kwenye smartphone tu na kwa sasa wanapatikana kwenye iphone, ipad, simu zote za android, windows phone na pia wanapatikana kwenye pc na laptop. Ukiwa na tango utapiga call buree na video call pia kuidownload click link hapo chini

https://tango.me

FRINGE

031913 1613 pigasimubur5

Hawa jamaa si kukubali calls tu bali pia wana video call wanakubali wao wanapatikana kwenye Symbian, androids na iphone. Kuidownload hapo chini click

kama una swali lolote usisite kuuliza chini

Mwandishi Hemedans Nassor Mchangiaji
Hemedans aka Chief Mkwawa, amekuwa mwandishi wa makala mbalimbali za teknolojia kuanzia kuanzishwa kwa Mtaawasaba. Kwa sasa ni mchangiaji kila anapopata nafasi
Maoni yako

Trending on Mtaawasaba

Receive Mtaawasaba notifications Click ‘Receive,’ then ‘Allow’ when prompted. Dismiss Receive