Vitu 6 vilivyogunduliwa na wanawake na kubadili dunia

Mwandishi Alexander Nkwabi

Tukiadhimisha siku ya kimataifa ya wanawake duniani, tutajaribu kuangazia baadhi ya michango ya wanawake katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia . Orodha ni ndefu na mambo ni mengi ambayo wanawake wameweza kuishangaza dunia katika nyanja za sayansi na teknolojia. Kwa leo tutakuletea gunduzi saba ambazo zimeibadili dunia jumla.

1. Mashine ya kuoshea vyombo (Dish Washer)

86bd35c526fca6593c7212d8e63a260e.png

Mwanamama Josephine Cochrane  mnamo mwaka 1886 alifanikiwa kuvumbua mashine ya kwanza ya kuoshea vyombo ambayo iliweza kuuzwa madukani. Mashine hiyo ambayo ilitumia presha kubwa ya maji, kigurudumu, kifaa cha kuchemshia maji, na kichanja cha kuwekea vyombo vikisubiri kukauka baada ya kuoshwa. Hata hivyo mwanamama huyu hakuweza kuutumia ugunduzi wake japo alifanya maisha ya wafanyakazi wake kuwa rahisi.

2. Dawa ya fangasi (Nystatin)

elizabeth_lee_hazen_rachel_fuller_brown_1950s
Dawa hii ya fangasi ambayo imesaidia mamilioni ya watu duniani kote, ni zao la ugunduzi wa wanawake wawili Elizabeth Lee Hazen na Rachel Fuller Brown ambao walikuwa wakifanya utafiti juu ya bakteria ambao walikuwa wanaua fangasi. Dawa hiyo waliipa jina la Nystatin kwa heshima ya mji waliokuwa wanatoka New York State.
Dawa hii imekuwa msaada mkubwa kutibu fangasi wa aina nyingi ikiwemo muwasho utakanao na nepi kwa watoto, fangasi wa ukeni kwa wanawake na aina zingine.

3. Boya la kuokolea maisha (The life raft)

Life_raft-e1432759820375

Boya hili liligunduliwa na mwanamama Maria Beasely mnamo mwaka 1882 baada ya siku moja kutazama baharini na kusema “watu hawatakiwi kufa kwenye chombo cha usafiri wa maji” kisha akabuni kifaa hicho ambacho kinaendelea kutumika mpaka leo japo kinafanyiwa maboresho ya hapa na pale.

4. Bomba la sindano

6-inventions

Bomba la sindano ni moja ya maajabu ya matibabu ya kisasa, mnamo mwaka 1899 mwanamama Letitia Geer alibuni bomba la sindano ambalo liliweza kushikwa mkono mmoja.

5. CCTV

020516-b-real-achievement-things-you-didn-t-know-were-invented-by-a-black-woman-security-camera

Kutokana na tatizo la wizi lililokithiri na polisi kuwa wazito katika kabiliana na wezi katika jiji la New York, mnamo mwaka 1969 Mwanamama Marie Van Brittan Brown alibuni mfumo wa ulinzi kwa kutumia kamera ambao unamruhusu mtumiaji kuona kinachoendelea kupitia kwenye runinga akiwa ndani ya nyumba. Ugunduzi wake ndio mwanzo wa mifumo ya kisasa ya CCTV inayotumika majumbani na polisi mpaka sasa.

6. Programu ya kompyuta

grace-hopper-1

Mnamo mwaka 1944 Dr. Grace Hopper alifanya ubunifu wa kompyuta katika chuo cha Havard iliyopewa jina la Mark I, kompyuta hii iliyokuwa na uzito wa tani tano na ukubwa wachumba kizima.  Yeye ndio mwanzilishi wa neno “bug” akimaansha tatizo lililo kwenye programu ya kompyuta na neno “debugging” baada kuwa kuwatoa dudu washa waliokuwa wameingia ndani ya kompyuta hiyo.

Mama huyu programa wa kompyuta ndie mbunifu wa lugha ya kompyuta ya COBOL (kirefu chake ni COmmon Business-Oriented Language) ambayo mpaka leo hii bado inatumika.

Mjadala kuhusu wanawake waliofanya mambo makubwa katika nyanja za sayansi na teknolojia nchini na hata nje ya nchi unaweza kuendelea hapo chini kwenye box la maoni. Tupe maoni yako pia kwenye mitandao ya kijamii kama Twitter, facebook na Instagram kupitia akaunti yetu ya mtaawasaba.

Mwandishi Alexander Nkwabi Mhariri
Mitandao ya Kijamii
Alex ni mhariri mwandamizi hapa Mtaawasaba.com, kwa kipindi kirefu amekuwa akivutiwa na mfumo endeshi wa Android na michezo ya kompyuta. Alex akiwa haandiki hapa Mtaawasaba basi hupendelea kupiga picha, kusafiri na kusoma vitabu.
Maoni yako

Trending on Mtaawasaba

Receive Mtaawasaba notifications Click ‘Receive,’ then ‘Allow’ when prompted. Dismiss Receive