WhatsApp wazindua kipengele cha picha na video zinazofutika baada ya kuzifungua

Mwandishi Alexander Nkwabi

Watumiaji wa WhatsApp sasa wanaweza kutuma picha na video ambazo zinaweza kupotea baada ya kuonwa mara moja (View Once), kipengele hiki kimeongezwa kama njia mojawapo ya kuboresha faragha. 

 

Imethibitishwa huduma hii mpya ya View Once itaanza kutumika wiki hii.

WhatsApp wamedai kuwa hii ni njia salama kutuma na kupokea taarifa nyeti bila kuhifadhiwa au kuonwa zaidi ya mara moja kwani watumiaji watakaokuwa hewani pekee ndio wataweza kuona video na picha za namna kabla hazijafutika

Whatsapp View once

Tayari mitandao kadhaa ya kijamii kama Snapchat, Telegram na Instagram imekuwa na huduma kama hii ambayo huwaruhusu watumiaji kutuma jumbe zinazojifuta mara baada ya kufunguliwa.

Kutoka kwenye blogu ya mtandao huu wa kijamii unaomilikiwa na kampuni ya Facebook iliandikwa,

 

“ kupiga picha na video imekuwa ni sehemu ya Maisha yrtu, japo si kila tunachoshea lazima kibaki kwenye rekodi za kidijitali moja kwa moja,

 

Ndio maana leo tunaachia hiki kipengele kipya cha kuona mara moja picha na video ambazo zitatoweka mara baada ya kuziona mara moja, hii itawapa watumiaji uwezo Zaidi wa kusimamia faragha zao”

Mara tu picha au video itakapofunguliwa na kisha ki=utoweka, mahala palipokuwepo picha/video hiyo pataandikwa “opened” ili kuondoa mkanganyiko, wameandika WhatsApp.

 

Hata hivyo kwa maandishi madogo sana wameandika “kipengele hiki hakita zuia wat uku screenshot picha kabla haijafutika”.

 

Una maoni gani kuhusu huduma hii mpya iloachiwa na WhatsApp? Andika maoni yako hapo chini.

Mwandishi Alexander Nkwabi Mhariri
Mitandao ya Kijamii
Alex ni mhariri mwandamizi hapa Mtaawasaba.com, kwa kipindi kirefu amekuwa akivutiwa na mfumo endeshi wa Android na michezo ya kompyuta. Alex akiwa haandiki hapa Mtaawasaba basi hupendelea kupiga picha, kusafiri na kusoma vitabu.
Maoni yako

Trending on Mtaawasaba

Receive Mtaawasaba notifications Click ‘Receive,’ then ‘Allow’ when prompted. Dismiss Receive