Yahoo imenunua application iliyotengenezwa na Kijana mwenye umri wa miaka 17 kwa mamilioni ya dola

Mwandishi Alexander Nkwabi

Ni mbunifu wa app ya habari iitwayo ‘Summly’, kijana huyo mwenye umri wa miaka 17 amejikuta amekuwa milionea baada ya Yahoo kuinunua application yake.

Japo haijulikani ni kiasi gani hasa alicholipwa lakini ni mamalioni ya dola.App hiyo itaanza kutumika kwenye products za Yahoo. Summly huchukua habari za mtandaoni na kuzifupisha kuwa na maneno 400 ambazo ni rahisi kusomwa kwenye simu za mkononi.

Sub yahoo articlelarge

Pia, mtoto huyo atakuwa mwajiriwa wa Yahoo mwenye umri mdogo zaidi.Nick aliitengeneza app hiyo akiwa na umri wa miaka 25 na kupata uwekezaji kutoka kwa kampuni ya bilionea wa Hong Kong, Li Ka Shing iitwayo Horizons Ventures na kupata shavu kutoka kwa mastaa kama Stephen Fry, Yoko Ono na Ashton Kutcher waliowekeza kwa zaidi ya paundi milioni moja.

App hiyo kwaajili ya simu za iPhone ilianzishwa December 2012 na Summly ilifanya kazi na mitandao zaidi ya 250 duniani.

Avatar of alexander nkwabi
Mwandishi Alexander Nkwabi Mhariri
Mitandao ya Kijamii
Alex ni mhariri mwandamizi hapa Mtaawasaba.com, kwa kipindi kirefu amekuwa akivutiwa na mfumo endeshi wa Android na michezo ya kompyuta. Alex akiwa haandiki hapa Mtaawasaba basi hupendelea kupiga picha, kusafiri na kusoma vitabu.
1 Comment

Trending on Mtaawasaba

Receive Mtaawasaba notifications Click ‘Receive,’ then ‘Allow’ when prompted. Dismiss Receive