Google kutengeneza Miwani Janja (Smartglasses)

Alexander Nkwabi Maoni
Kampuni ya Google kutengeneza Miwani Janja (Smartglasses) mpya. Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinadai Kampuni ya Google iko mbioni kuingia katika soko la Miwani janja za AR na imeanza majaribio ya kutengeneza AR Glasses zake.

Mpaka sasa kampuni za simu na mitandao ya kijamii za Snapchat, Ray Ban, Meta, TikTok, Xiaomi, Oppo na Huawei zimeshatoa miwanijanja zao mpya ambazo zina uwezo wa Augmented Reality. Na pia kampuni ya Apple pia ipo katika matengenezo na inaunda Smart Glasses zake.

Mwaka juzi Google iliinunua kampuni ya North ambayo inayohusika na kutengeneza smart glasses za Focals 2.0. Google inajipanga kujaribu kutengeneza smart-glasses zake na ipo katika mchakato wa kutengeneza na inategemewa itatoka mwaka huu.

Faida kubwa ya miwani janja za Google ni kuwa zinakuja na Google Lens, Google Assistant na mfumo mzuri wa AR hivyo itakuwa ni miwani janja na yenye akili kwa kuunganisha na mfumo wa Google.

Itakuwa ni maalum kwa wanafunzi, designers, madaktari na wataalam mbalimbali. Tofauti na VR kama za Sony na Meta; AR (Augmented Reality) glasses ni simple na inatumia mazingira yaliyopo kuongeza details za ziada kama vile infos, notifications, directions na mtu anaona mbele kama kawaida huku akiwa anaona details za ziada.

Kwa sasa kampuni kubwa za Tech zinajikita kwenye soko la miwani janja za AR baada ya Snapchat, Ray Ban na Facebook kufanikiwa katika AR Glasses.

Mwandishi Alexander Nkwabi Mhariri
Mitandao ya Kijamii
Alex ni mhariri mwandamizi hapa Mtaawasaba.com, kwa kipindi kirefu amekuwa akivutiwa na mfumo endeshi wa Android na michezo ya kompyuta. Alex akiwa haandiki hapa Mtaawasaba basi hupendelea kupiga picha, kusafiri na kusoma vitabu.
Maoni yako